Sanaa za asili


Kipengele hiki kinajumuisha mavazi ya aina mbali mbali wanayotumia katika shughuli za jamii ya Wazanzibar kutokana na maendeleo ya jamii na maingiliano ya watu wetu na mataifa mengine Mavazi kama baibui la uzi na kanga kwa wanawake na kanzu na kofia za kiua na koti kwa wanaume yamekuwa yakiutambulisha utamaduni wetu.


MAVAZI HALISI YA MZANZIBARI
Ni moja ya mavazi yanayoutambulisha utamaduni wa mzanzibari

DHANA ZA UTAMADUNI

MILA

Dhana hii hujumuisha vipengele vya malezi, tiba za asili, mazindiko, ramli na utabiri, kinga, harusi, vifo, mirathi na kadhalika Huu ni muhimili mwengine wenye nguvu katika kuelezea utamaduni wa Zanzibar. Kupitia mila jamii inapata uwezo wa kuufufua, kuuhuisha, kuimarisha, kuuenzi na kuuendeleza utamaduni wao.

DESTURI

Kipengele hiki huhusisha kawaida za jamii kama vile; maamkizi, kutembeleana, kusaidiana, hishima, adabu na maadili mema. Kwa ujumla desturi inapojikita na kuimarika katika jamii hugeuka na kuwa mila. Ndipo Waswahili wakasema Kawaida ni kama sheria.

ITIKADI

Kipengele hiki huhusisha mambo ya imani za kiroho, kijadi na kisiasa. Masuala ya ibada, tambiko na mizimu zinaingia katika uwanja huu.




SANAA ZA ASILI

Hii hujumuisha shughuli zote zinazofanywa na binaadamu kwa kutumia ustadi wake. Kwa ujumla, sanaa hugawiwa katika mafungu makuu matatu: sanaa za maonesho, sanaa za ghibu kama muziki wa ala tupu na sanaa ya utendaji (uhandisi) ambazo tumezowea kuziita sanaa za ufundi.


MAVAZI YA MZANZIBARI

Kipengele hiki kinajumuisha mavazi ya aina mbali mbali wanayotumia katika shughuli za jamii ya Wazanzibar kutokana na maendeleo ya jamii na maingiliano ya watu wetu na mataifa mengine Mavazi kama baibui la uzi na kanga kwa wanawake na kanzu na kofia za kiua na koti kwa wanaume yamekuwa yakiutambulisha utamaduni wetu.

LUGHA

Kipengele hiki kinajumuisha lahaja zote za lugha ya kiswahili ambayo jamii inazitumia katika mawasiliano na fasihi zote mbili andishi na simulizi ambazo ni zao la jamii yenyewe inayohusika na mila za watu.